Wanafunzi shule ya Msingi Kakola hatarini kuugua magonjwa ya tumbo na Kipindupindu. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Thursday, June 9, 2016

Wanafunzi shule ya Msingi Kakola hatarini kuugua magonjwa ya tumbo na Kipindupindu.



Wanafunzi wa shule ya Msingi Kakola  iliyoko katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama Shinyanga wako hatarini kupatwa na magonjwa ya tumbo na kipindupindu kufuatia vyoo vichache vya shule hiyo kufurika hali ambayo inadaiwa kusababisshwa na baadhi ya viongozi wa kata na kijiji kubadilisha matumizi ya fedha za ujenzi wa choo cha shule hiyo zilizotolewa na Halmashauri ya Msalala.
Wakizungumzia hali hiyo baadhi ya wakazi wa kijiji cha kakola wamewalalamikia baadhi ya viongozi wa kata na kijiji kuficha baadhi ya nyaraka za miradi ya maendeleo na kutowasomea taarifa ya mapato na matumizi huku wakimtaka mwenyekiti wa kijiji na diwani wa kata hiyo Bw.John Shiganga kutamka hadharani ni lini choo cha shule hiyo kitajengwa na kukamilika.
 
Akijibu tuhuma hizo kwa niaba ya diwani anayelalamikiwa kubadilisha matumizi ya fedha za ujenzi wa choo cha shule ya Kakola  mtendaji wa kijiji hicho ambaye naye anadaiwa  kushirikiana na diwani kukiuka makubaliano Bw.Ramadhani Madefe amedai amesema alichotekikeleza ni maagizo aliyopewa huku mwenyekiti wa kijiji cha kakola Bw.Emmanuel Bombeda akilazimika kuwatuliza wananchi waliopatwa na hasira baada kuona diwani wao hakufika katika mkutano huo kujimbu malalamiko yao.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin