nyula blog: MATUKIO

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...
Showing posts with label MATUKIO. Show all posts
Showing posts with label MATUKIO. Show all posts

Thursday, September 15, 2016

Madereva kutoka Tanzania watekwa nchini DRC.





Serikali imepokea taarifa za kutekwa kwa malori 12 katika eneo la Namoyo Jimbo la Kivu Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, jana tarehe 14 Septemba 2016. Kati ya malori hayo nane yanamilikiwa na mfanyabiashara wa Kitanzania, Bw. Azim Dewji na mengine yanamilikiwa na wafanyabiashara kutoka Kenya.

Kwa taarifa zilizopatikana watekaji ni kikundi cha waasi cha MaiMai ambao baada ya kuyateka magari hayo, waliwashusha madereva na kuwapeleka porini na kisha kuteketeza kwa moto malori manne ambayo yote ni ya Bw. Dewji. Waasi hao wametoa saa 24 kuanzia jana saa 10 jioni walipwe fedha kiasi cha Dola za Kimarekani 4,000 kwa kila dereva ili waweze kuwaachia. 


Wametishia kuwaua mateka hao endapo hawatalipwa kiasi hicho cha fedha wanachokitaka itakapofika saa 10 jioni leo. Katika tukio hilo, madereva wawili wa Kitanzania wamefanikiwa kutoroka ambao ndio waliosaidia kutoa taarifa rasmi kuhusu tukio hilo.

Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeshachukua hatua za awali za kuwasiliana na Serikali ya DRC ili kuhakikisha kuwa madereva hao wanaachiwa haraka iwezekanavyo wakiwa salama kabisa.

Tukio hili ni la pili kutokea katika miaka ya hivi karibuni ambapo mwaka 2015 Mashekhe kutoka Tanzania walitekwa nchini DRC lakini kwa ushirikiano wa Serikali hizi mbili zilifanikisha mashekhe hao kuachiwa huru bila madhara yoyote.

Serikali ingependa kuushauri Umma wa Watanzania hususan wafanyabiashara kuomba taarifa ya hali ya usalama kwa maeneo yenye matatizo ya kiusalama kama Mashariki ya Congo hususan Kivu ya Kusini kabla ya kusafiri kwenda maeneo hayo.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Dar es Salaam, 15 Septemba 2016.

Kijana Anyofolewa Ulimi na Mwanamke Wakati Wakipigana Denda




Mkazi wa Mandewa, Manispaa ya Singida, Said Mamba (24), amelazwa katika hospitali ya mkoa mjini Singida baada ya kung’atwa theluthi tatu ya ulimi wake na mwanamke waliyekuwa wakinyonyana ndimi. 

Tukio hilo la aina yake lilitokea Septemba 12, saa 3:30 usiku wa sikukuu ya Idd el Hajj. 
Mamba, ambaye hawezi kuzungumza ametoa maelezo ya tukio hilo kwa njia ya maandishi. 

Alisema siku ya tukio alikutana na mwanamke huyo kwenye grosari iliyopo eneo la Mandewa na baadaye mwanamama huyo alimwomba amsindikize nyumbani kwake. 
“Nilikubali kumsindikiza, tukiwa njiani aliniomba tufanye mapenzi. Nilipokataa alinilazimisha na baada ya kuona sitaki aliomba tuagane kwa kunyonyana ndimi, nilikubali ombi hilo,” alisema. 
Mamba alisema wakati wakiendelea, mwanamke huyo alianza kumvua mkanda wa suruali lakini alimzuia ndipo alipomng’ata ulimi na kuondoka na kipande. 
Mzazi wa Mamba, Fatuma Alli alisema alipata taarifa ya tukio hilo baada ya siku tatu na kwamba, siku hiyo hiyo mume wa mwanamke aliyetenda kitendo hicho alikwenda kwake akieleza kijana huyo alijaribu kumbaka mkewe. 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Peter Kakamba, alisema hana taarifa za tukio hilo. 

Daktari wa meno wa hospitali hiyo, Dk Hamisi Kakandilo alisema ulimi wa kijana huyo hauwezi kutibika isipokuwa kuusafisha ili asipate maambukizi. 

“Hata kama kipande kilichotolewa kingepatikana kisingeweza kushonwa,” alisema.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 16




==>Magazeti mengine yataweka ikifika saa 12 Asubuhi....Endelea kuutembelea ukurasa huu

Thursday, September 8, 2016

Magazeti ya Tanzania September 9, 2016


20160909_045706
20160909_045716
20160909_045724
20160909_045732
20160909_045748
20160909_045757
20160909_045807
20160909_045816
20160909_045833
20160909_045843
20160909_045856
20160909_045903
20160909_045912
20160909_045921
20160909_045931
20160909_045938
20160909_045951
20160909_045958
20160909_050008
20160909_050016
20160909_050028
20160909_050036
20160909_050044
20160909_050051
20160909_050103
20160909_050110
20160909_050118
20160909_050125
20160909_050135
20160909_050142
20160909_050207
20160909_050214
20160909_050236
20160909_050245

Wednesday, September 7, 2016

Magazeti ya Tanzania September 8, 2016.


20160908_050651
20160908_050700
20160908_050709
20160908_050716
20160908_050733
20160908_050741
20160908_050756
20160908_050804
20160908_050816
20160908_050824
20160908_050839
20160908_050847
20160908_050855
20160908_050904
20160908_050916
20160908_050924
20160908_050934
20160908_050942
20160908_050953
20160908_051001
20160908_051010
20160908_051017
20160908_051030
20160908_051036
20160908_051048
20160908_051056
20160908_051106
20160908_051115
20160908_051124
20160908_051131
20160908_051143
20160908_051150
20160908_051230
20160908_051239