Walengwa 164 waondolewa Tasaf,kwa kutokidhi vigezo. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Thursday, June 9, 2016

Walengwa 164 waondolewa Tasaf,kwa kutokidhi vigezo.



Halmashauri ya wilaya ya Karagwe imewaondoa kwenye mpango wa kunusuru kaya masikini unaotekelezwa na mfuko wa maendeleo ya jamii(Tasaf III)walengwa 164,kutokana na walengwa hao kubainika kutokidhi vigezo vya mfuko huo.
Walengwa hao ambao awali walikuwa wakipokea ruzuku inayotolewa na mfuko huo,wameondolewa mara baada ya uhakiki wa walengwa halali wanaopaswa kupokea ruzuku hiyo,uliofanywa na wataalamu wa idara mbalimbali kutoka ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri hiyo.
 
Akiongea ITV Afisa Mshauri na Mfuatiliaji wa Tasaf wilaya ya Karagwe Elias Sowani,idadi hiyo ya walengwa waliondolewa kwenye mpango imetokana baada ya uhakiki wa kina,na kufanikiwa kubaini baadhi ya walengwa hawakuwa na sifa zinazotambuliwa na mfuko huo,huku wengine wakiwa na kasoro za kutokuwa raia wa nchi ya Tanzania.
 
Sowani amesema kuwa wengine walibainika kuwa ni wajumbe wa Serikali za vijiji vyao,huku  baadhi yao wakitolewa moja kwa moja kwenye orodha kutokana na sababu za vifo.
 
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin