Zaidi ya watu miatatu wavamia hekari mianne za mwekezaji wilayani Arumeru. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News

Wednesday, May 11, 2016

Zaidi ya watu miatatu wavamia hekari mianne za mwekezaji wilayani Arumeru.



Zaidi ya watu miatatu wakazi wa kijiji cha Mlangarini wilaya ya Arumeru wakiwa na mashoka jembe nyundo na mafekeo wamevamia zaidi ya hekari mianne za shamba la mwekezaji kugawana kupanda mahindi na kutenga maeneo ya huduma muhimu wakidai shamba ilo limekaa muda mrefu bila kutumika huku wananchi wakikosa maeneo ya kilimo na huduma.
ITV ilifika katika kijiji cha Mlangarini na kushuhudia mamia ya watu wakiwa na zana za jadi wakifeka kulima na kupanda mahindi kwenye maeneo waliyo jigawia huku wakiahinisha maeneo ya huduma muhimu na kudai wananchi wanateseka huku watu wachache wakimiliki maeneo makubwa bila kuyatumia hivyo wameamua kugawana. 
 
Wanawake kutoka katika kijiji hicho wameeleza namna wanavyo teseka kwa kukodishwa mashamba hayo kwa ghalama ya juu na mashariti magumu na kwamba wamefikisha kero hiyo ngazi mbalimbali bila mafanikio. 
 
Wazee wanao kadiliwa kuwa na umri wa miaka sabini nawo wakatoa historia fupi ya mashamba hayo huku wakiunga mkono hatua hiyo na katika tukio ilo hapakuwepo kiongozi yoyote wa serikali na juhudi za kuwatafuta viongozi wa wilaya ya Arumeru pamoja na mwekezaji zinaendelea.
 
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin