Upinzani walitaka Bunge kuwaweka hadharani wahujumu uchumi bila kujali nyadhifa wala vyama vyao. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Wednesday, May 18, 2016

Upinzani walitaka Bunge kuwaweka hadharani wahujumu uchumi bila kujali nyadhifa wala vyama vyao.


Wabunge wameendelea kuijadili bajeti ya wizara ya ujenzi,uchukuzi na Mawasiliano  huku kiongozi mkuu wa kambi ya upinzani Bungeni Mhe.Freeman Mbowe akiliambia bunge hilo kuwa msimamo wa kambi hiyo ni kumtaja hadharani na kumshutumu mtu yeyote ambaye alishiriki ama anashiriki katika kulihujumu taifa bila kujali kama yupo Serikalini ama kambi ya upinzani.
Kiongozi huyo mkuu  wa kambi hiyo ya upinzani amesema hayo kufuatia wabunge kupitia chama cha mapinduzi kumshutumu aliyekuwa Waziri mkuu wakati uuzaji wa nyumba hizo  za Serikali Mhe.Edward Lowasa ambaye sasa ni mjumbe wa kamati kuu ya chadema kuwa naye alishiriki katika uuzaji wa nyumba hizo kwani Rais wa sasa Dr.John Magufuli  alikuwa waziri wa ujenzi  na  Mhe.Lowasa alikuwa bosi wa Dr.Magufuli kama Waziri Mkuu.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin