Kamati ya ulinzi na usalama yanasa Luninga (TV) 288 zilizofichwa chooni katika Bandari ya Kilwa. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Wednesday, May 18, 2016

Kamati ya ulinzi na usalama yanasa Luninga (TV) 288 zilizofichwa chooni katika Bandari ya Kilwa.


.
Serikali ya wilaya ya Kilwa mkoani Lindi imemuagiza mkuu wa upelelezi wa wilaya hiyo kuchukua maelezo ya kina , ikiwa ni pamoja na kuwahoji maafisa wa TRA bandari na walinzi wa bandari ya Kilwa baada ya Luninga 288 aina ya flat screen kukutwa zikiwa zimefichwa katika choo no 3 na namba nne bandarini.
Luninga hizo zimetokana na shehena ya mzigo wa mfanyabiashara aliyefahamika kwa jina la Teachea kukamatwa  katika Bandari ya Kilwa ukitokea zanziba baada ya kutiliwa mashaka haujalipiwa kodi na hivyo kuhifadhiwa katika ghala la bandari hiyo.
 
Akizungumza mara baada ya kuvamia ghafla bandarini  baada ya kupata taarifa za kuwapo mzigo huo  Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Juma Njuwayo anasema  ripoti za kiiteljensia zinaonyesha kuna wizi katika bandari hiyo unaofanywa na maafisa wa bandari hiyo.
 
hata hivyo Meneja wa TRA wilayani  Kilwa Titus Shindano ameonyesha kushangazwa na hilo na kusema mara zote amekuwa akionyeshwa mzigo uliyopo ghalani na si vinginevyo.
 
 
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin