Polisi watanda mitaa ya kariakoo jijini DSM kuwadhibiti wamachinga wasipange bidhaa zao chini. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News

Wednesday, May 11, 2016

Polisi watanda mitaa ya kariakoo jijini DSM kuwadhibiti wamachinga wasipange bidhaa zao chini.



Jeshi la Polisi limetanda mitaa yote ya Kariakoo jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuwadhibiti wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama wamachinga wasipange bidhaa zao chini hatua ambayo wamachinga hao wameipinga kwa kuanza kurusha mawe ovyo na kusababisha baadhi ya wamiliki wa maduka kufunga maduka yao na ili kuepousha uwezkekano wa kutokea mdhara zaidi.
ITV ilifika mitaa ya kariakoo na kusuhudia gari za polisi zikipita huku na kule na baadhi ya wamachinga hao wakizomea na kupiga miluzi ovyoovyo hataua ambayo ilikuwa kama ni ishara ya kuwachokoza polisi ambao kila mara walilazimika kufuata makundi mbalimbali ya watu na kuwatawanya.
 
Baadhi ya wafanyabishara hao wamesema siyo kwamba wanapinga kuondoka kariakoo bali ni namna ambavyo wanaondolewa kama vile wao ni takataka.
 
Hata hivyo baadhi ya wafanyabiashara hao wamepongeza kitendo cha kuondolewa katia mitaa hiyo kwani kwa sasa mandhari yamebadilika na hata magari pamoja na watu wanapita katika njia zao kwa urahisi zaidi.
 
Kwa upande wake mwenyekiti wa jumuiya ya wafanyabiashara nchini Bw Filimini Romano amelani Kitendo cha baadhi ya wamachinga  kurusha mawe na kusababisha baadhi ya maduka kufungwa na kusema kitendo hicho siyo cha kiungwana.
 
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin