Mjane wa miaka 80 arejeshwa kwenye nyumba yake iliyotaka kuuzwa mkoani Arusha. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Sunday, May 15, 2016

Mjane wa miaka 80 arejeshwa kwenye nyumba yake iliyotaka kuuzwa mkoani Arusha.


Hatimaye mama mjane wa zaidi ya miaka 80 aliyekuwa anaishi kwa msaada wa majirani baada ya kutolewa nje ya nyumba yake na watu wanataka kuiuza amerudishiwa nyumba yake na amekishukuru kituo cha ITV kwa kutoa taarifa zilizowezesha serikali kuchukua hatua.
Jaribio la kutaka kuuza nyumba ya mama huyo Bi Khadija Issa lilifanyika mwishoni mwa mwezi April mwaka huu katika eneo la Kaloleni jijini Arusha baada ya kundi la watu wakiwa na askari wa kampuni binafsi za ulinzi walivamia nyumba yake na kumtoa nje na kufunga nyumba hiyo.
 
Pamoja na jaribio hilo kushindwa baadhi ya ndugu na majirani wa mjane huyo wameiomba serikali kuendelea kuwachukulia hatua baadhi ya watu wanaoendesha kampeni za kudhulumu mali za wajane na wagane. 
 
Mlezi wa mjane huyo Bw Isumail Issa amelalamikia uharibifu na wizi  wa mali zenye thamani ya dola elfu 30 uliofanyika wakati wa jaribio la  kupora nyumba ya mjane huyo. 
 
Mama huyo mjane aliyetolewa ndani ya nyumba yake hiyo kabla ya kurejea kwa muda wote amekuwa akiishi kwa majirani akitegemea  misaada ya wasamaria wema.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin