Baadhi ya wabunge wamesema miundombinu rafiki itaifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Monday, May 9, 2016

Baadhi ya wabunge wamesema miundombinu rafiki itaifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda.



Baadhi ya wabunge wamesema azma ya serikali ya awamu ya tano kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda itatimia kama serikali ikiweka miundombinu rafiki ya utekelezaji wa hilo huku umoja wa wabunge wanawake ukilaani kauli ya kudhalilishwa wanawake iliyotolewa wiki iliyopita bungeni hapo.
Wakichangia bajeti ya wizara ya viwanda, biashara na uwekezaji, wabunge hao wamesema ipo haja ya mapungufu yaliyopo katika sekta ya viwanda na biashara nchini yakafanyiwa kazi kwani yanafahamika ila utatuzi wake umekuwa wa kusuasua. 
Baadhi ya wabunge kutoka vyama vya upinzani wamesema serikali inatakiwa kuweka kipaumbele katika kufufua viwanda vilivyokufa kama ilivyoahidi kwani watanzania bado wanaimani kuwa vikifufuliwa vitaweza kufanya vyema. 
 
Naye waziri wa wizara hiyo Charles Mwijage amesema kila anachokisema bungeni atakitekeleza kwani yeye ni mtu wa vitendo na siyo maneno na kama kuna mbunge aamini hilo amtafute na aeleze anataka mwekezaji wa sekta gani na atampata baada ya muda mfupi huku akitoa baadhi ya maagizo kwa watendaji wa chini wa wizara yake.
 
Awali bungeni hapo mwenyekiti wa umoja wa wabunge wanawake Magreth Sitta aliwasilisha maelezo binafsi ya umoja huo na kulaani kauli ya udhalilishaji waliyoambiwa wanawake wa vyama vya upinzani viti maalum kuwa wabunge mpaka wawe na uhusiano wa kimapenzi na viongozi wa vyama vyao.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin