Tukio hilo ambalo limesababisha wagonjwa watatu ambao wamelazwa
katika kituo hicho cha afya maarufu kama hospitali ya Sungusungu
kujeruhiwa vibaya kwa kipigwa risasi, imeelezwa na baadhi ya viongozi wa
vijiji katika eneo hilo kuwa askari polisi walianza kurusha risasi
baada ya kutofautiana na familia katika kuchukua mwili wa kijana huyo
Jackison Mwita.
Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Tarime vijijini Mh John Heche
ambaye ametembelea mji wa Nyamongo kufuatia tukio hilo, ameonesha
kusikitishwa kwa askari polisi hao kuua wananchi kwa risasi kisha
kusababisha vurugu hizo ambazo pia zimesababisha uharibifu mkubwa katika
kituo hicho cha afya.
Naye mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama Bw Gloriuos Luoga
ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Tarime amesema baada serikali kupokea
taarifa rasmi ya uchunguzi wa jopo la madaktari, serikali itaunda tume
ili kujua kiini cha tukio hilo.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini