SUMATRA yatangaza nauli zitakazotumika katika uendeshaji wa mabasi yaendayo kasi jijini Dar es Salaam. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Monday, May 9, 2016

SUMATRA yatangaza nauli zitakazotumika katika uendeshaji wa mabasi yaendayo kasi jijini Dar es Salaam.



Mamlaka ya usafiri wa nchi kavu na majini SUMATRA imetangaza nauli zitakazotumika katika uendeshaji wa mabasi yaendayo haraka huku waendesha bodaboda na watumiaji wengine wa vyombo vya usafiri wakipigwa marufuku kupita katika barabara za mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam.
Umamuzi huo umekuja baada ya majadiliano ya ipi iwe bei ya nauli ya Mabasi hayo yaendayo haraka, ambapo siku 90 zilitosha kufikiwa kwa muafaka huku bodi ya SUMATRA ikiamini viwango hivi vya nauli ni rafiki kwa kila mtanzania. 
 
Mtendaji Mkuu wa DARTS Mhandisi Ronald Lwakatare, amesema kuanzia sasa hatua kali za kisheria zitaanza kuchukuliwa kwa mtumiaji yeyote wa chombo cha usafiri atakayepitisha gari, pikipiki, guta,au  baiskeli  katika barabara za mabasi yaendayo haraka.
 
Wakati usafiri mabasi yaendayo haraka ukitarajiwa kuanza muda wowote kuanzia sasa, baraza la madiwani la jijini la Dar es salaam  lililoketi Mei 2 mwaka huu limepitisha maazimio kadhaa yakiwemo ya kupinga ununuzi wa hisa zake katika shirika la UDA ambazo ni sawa na asilimia 51.
 
Wakazi wa jiji la Dar es Salaam wamepongeza juhudi kubwa za serikali za kuondoa foleni katika jiji hili la Dar es Salaam.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin