Zaidi
 ya wafanyakazi 150 wa kampuni ya China Railway Jianchang Engineering 
(CRJE), inayojenga miradi mikubwa ya majengo ya vitega uchumi katika 
maeneo ya Capripoint na Ghana jijini Mwanza, wamegoma kuingia kazini 
wakishinikiza kulipwa malimbikizo ya mapunjo ya mishahara yao ya miaka 
mitatu iliyopita pamoja na stahiki zao mbalimbali ikiwemo michango ya 
mfuko wa pensheni wa NSSF.
 
 
 
 
Wafanyakazi wa kampuni hiyo ya CRJE waliogoma kuingia kazini ni 
wale wanaojenga jengo la Rock City Shopping and More lililopo eneo la 
Ghana, ambalo ni mradi wa mfuko wa pensheni wa LAPF na wenzao 
wanaoendelea na mradi wa ujenzi wa hoteli ya kitalii yenye hadhi ya 
nyota tano ya ghorofa kumi na sita, ambayo ni kitega uchumi cha mfuko wa
 pensheni wa NSSF, mradi huo unatarajia kukamilika mwezi Novemba mwaka 
huu.
ITV pia imefika katika mradi wa uwekezaji mkubwa wa jengo la Rock 
City Shopping and More mtaa wa Ghana na kuwakuta wafanyakazi zaidi ya 70
 wakiwa wameweka chini zana zao za kazi ambapo baadhi ya wafanyakazi hao
 walikuwa na haya ya kusema kuhusiana na mgomo huo.
Katibu wa chama cha wafanyakazi wa migodi, nishati na ujenzi 
(STAMICO) kanda ya ziwa, Paterinusi Rwechungura amefika katika eneo la 
Capripoint na kuzungumza na wafanyakazi hao.
Meneja mradi wa kampuni ya CRJE Li bo, kupitia kwa mkalimani wake 
Bwani Bwakeha amesema wamezingatia madai ya wafanyakazi hao na taratibu 
za uhakiki wa malipo yao zilipangwa kuanza hii leo mchana kuanzia majira
 ya saa nane mchana.
 Download Video and Put Comment
 Toa Maoni Hapa Chini