Waziri wa Mali asili na utalii Prof. Jumanne
Maghembe amewataka askari wa kulinda wanyama pori katika hifadhi ya
wanyama ya Serengeti mkoani Mara kuwarudishia wananchi ng'ombe 6000
ambao walishikiliwa baada ya kuingia eneo la hifadhi eneo la Busega.
Waziri
amefikia uamuzi huo baada ya Mbunge wa Jimbo la Busega CCM Dkt
Rhaphael Chegeni ambaye ametaka kauli ya serikali kuhusiana na ng'ombe
ambao wanazuiliwa katika hifadhi hiyo.
''Mheshimiwa naibu spika ngombe wamezuiliwa wakati wao hawana akili na wanateswa bila malisho je serikali inachukua hatua gani ili wananchi wachukue mifugo yao?'' Ameuliza Dkt. Chegeni
Akijibu swali hilo waziri Maghembe amesema ng'ombe hao waachiwe mara moja ili kuleta mahusiano mazuri kati ya wananchi wanaozunguka hifadhi pamoja na serikali.
''Mheshimiwa naibu spika ngombe wamezuiliwa wakati wao hawana akili na wanateswa bila malisho je serikali inachukua hatua gani ili wananchi wachukue mifugo yao?'' Ameuliza Dkt. Chegeni
Akijibu swali hilo waziri Maghembe amesema ng'ombe hao waachiwe mara moja ili kuleta mahusiano mazuri kati ya wananchi wanaozunguka hifadhi pamoja na serikali.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini