Kocha msaidizi wa Yanga Juma Mwambusi amesema
watacheza kwa umakini na hawataidharau Prisons katika mchezo wa Mzunguko
wa pili wa ligi kuu unaotarajiwa kuchezwa hapo kesho Uwanja wa Sokoine
jijini mbeya.
Mwambusi
amesema anaifahamu Prisons ni timu nzuri na watahakikisha wachezaji wao
wanacheza kwa umakini ili waweze kuondoka na Pointi tatu.
Mwambusi amesema, mchezo huo ni muhimu kwao kushinda baada ya kufungwa 2-0 na Coastal Union na bado wanaamini kila mchezo ni fainali kwao ingawa wana kibarua kigumu cha kupata matokeo mazuri kwa wenyeji Tanznaia Prisons.
Mwambusi amesema, licha ya kumkosa beki wao Kelvin Yondani ana imani hakutakuwa na pengo kwani wamemwandaa mchezaji wa kucheza nafasi hiyo.
Yondani alionyeshwa kadi nyekundu katika mchezo uliopita dhidi ya Coastal Union ambako Yanga walifungwa ingawa inaongoza katika Msimamo wa Ligi hiyo kutokana na Pointi 39 sawa na Azam FC lakini zinatofautiana mabao ya kufunga na kufungwa.
Mwambusi amesema, mchezo huo ni muhimu kwao kushinda baada ya kufungwa 2-0 na Coastal Union na bado wanaamini kila mchezo ni fainali kwao ingawa wana kibarua kigumu cha kupata matokeo mazuri kwa wenyeji Tanznaia Prisons.
Mwambusi amesema, licha ya kumkosa beki wao Kelvin Yondani ana imani hakutakuwa na pengo kwani wamemwandaa mchezaji wa kucheza nafasi hiyo.
Yondani alionyeshwa kadi nyekundu katika mchezo uliopita dhidi ya Coastal Union ambako Yanga walifungwa ingawa inaongoza katika Msimamo wa Ligi hiyo kutokana na Pointi 39 sawa na Azam FC lakini zinatofautiana mabao ya kufunga na kufungwa.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini