Watu
watano wa familia moja wakiwemo watoto watatu katika mtaa wa Sume kata
ya Mwembesongo manispaa ya Morogoro wamenusurika kifo baada ya nyumba
wanayoishi kuangukiwa na ukuta wa uzio wa kituo cha mafuta cha total
usiku wakiwa wamelala.
ITV imefika katika eneo hilo na kushuhudia nyumba hiyo ikiwa
imebomoka kabisa upande wa nyuma ambapo majeruhi wa tukio hilo wameeleza
jinsi lilivyotokea huku wanafamilia wamelalamikia kulala nje kwa zaidi
ya siku tatu na hawajui hatima yao kutokana na mmiliki wa kituo hichi
kushindwa kuwasaidia na kwamba kabla ya ukuta huo kuanguka walitoa
tarifa lakini hazikufaniwa kazi.
Akizungumzia tukio hilo mwenyekiti wa mtaa wa Sume Hamis Totoro
amesema tukio hilo limetokea majira ya usiku ambapo majeruhi
waliwahishwa hospitali ya rufaa ya mkoa Morogoro pamoja na hali zao
kuendelea vizuri lakini mmoja wao ambaye ni mzee amehamishiwa katika
hospitali ya Agakan jijini Dar es Salaam kwa matibabu zaidi.
Kufuatia tukio hilo ITV imemtafuta mmiliki wa kituo hicho cha
mafuta cha Total bila mafanikio baada ya simu yake kuita bila kupokelewa
ingawa pia wafanyakazi wa kituo hicho wameshindwa kutoa ushirikiano kwa
waandishi wa habari huku wakiwazuiya kupigapicha kituo hicho.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini