Wananchi zaidi ya 100 wilayani kalambo mkoani Rukwa, watapeliwa ardhi yenye ukubwa wa zaidi ya ekari 1,700. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Thursday, June 9, 2016

Wananchi zaidi ya 100 wilayani kalambo mkoani Rukwa, watapeliwa ardhi yenye ukubwa wa zaidi ya ekari 1,700.



Wananchi zaidi ya mia moja wa kijiji cha Kachele kata ya Kisumba wilayani Kalambo mkoani Rukwa, wamelalamikia kitendo cha kitapeli na kilichojaa dhuluma walichofanyiwa, na kujikuta wakipoteza ardhi yao yenye ukubwa wa zaidi ya ekari 1,700, na sasa wanatangatanga kijijini hapo kama wakimbizi wakikosa hata maeneo ya kufanyia shughuli zao za kilimo.
Wakiongea kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji chao cha Kachele wilayani Kalambo, wananchi hao wamesema wamejikuta wakitapeliwa na kudhulumiwa na baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu, na hatimaye ardhi yao kuishia mikononi mwa mtu anayejiita mwekezaji kutoka mkoani Arusha, 
na wao kukosa kabisa maeneo ya kilimo huku baadhi ya wanaume wakiuza maeneo yao bila ya kushirikisha familia zao.
 
Mkuu wa wilaya hiyo ya Kalambo Bw. Wailman Ndile, akiongea na wananchi hao wa kijiji cha Kachele amemuagiza mwekezaji huyo aliyenunua shamba hilo lenye ukubwa wa zaidi ya ekari 1,700, afike ofisini kwake akiwa na watu wote waliomuuzia eneo hilo, na pia akiwa na muhtasari wa mkutano mkuu wa kijiji ulioidhinisha kununua eneo hilo.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin