Mkoa wa Lindi waweka mkakati wa makusudi kudhibiti kilimo cha ufuta ili kuepusha uharibifu wa misitu na mazingira. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Thursday, June 9, 2016

Mkoa wa Lindi waweka mkakati wa makusudi kudhibiti kilimo cha ufuta ili kuepusha uharibifu wa misitu na mazingira.



Serikali mkoani Lindi imeweka mkakati wa makusudi kudhiti kilimo cha ufuta ili kuepusha uharibifu wa misitu na mazingira unaotokana na ukataji miti hovyo wakati wa kuandaa mashamba kwa ajili ya kupanda ufuta.
Mkuu wa mkoa wa Lindi Godfrey Zambi ametoa kauli hiyo mjini Lindi wakati wa hafla ya kupokea tuzo ya kimataifa ya mazingira aliyoshinda mkurugenzi wa taasisi ya uhifadhi ya mpingo, Makala Jasper Jijini London na kukabidhiwa na binti wa malkia wa uingereza, shindano lililokuwa na washindani zaidi ya 130 kutoka nchi mbalimbali duniani ambapo makala ameshinda tuzo hiyo kutokana na kazi kubwa anayoifanya katika kuongoza taasisi ya mpingo kwenye usimamizi wa mazingira na maendeleo endelevu ya wananchi na jamii.
 
Kwa upande wao baadhi ya viongozi wa wilaya za mkoa wa Lindi pamoja na wananchi wamesema tuzo hiyo inayotolewa na mfuko wa kimataifa wa uhifadhi wa Whitley wenye makao yake makuu nchini Uingereza yenye hadhi ya juu duniani ambayo ni ya kwanza kutolewa kwa nchi za afrika itakuwa kichocheo kwa vijiji vya mkoa wa Lindi kuongeza kasi ya uhifadhi na kutilia mkazo uvunaji endelevu wa misitu ya vijiji.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin