TCRA yazima simu feki 630.000 katika kampeni yake ya kuondoa simu feki sokoni. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Friday, June 17, 2016

TCRA yazima simu feki 630.000 katika kampeni yake ya kuondoa simu feki sokoni.



Mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA imezima namba za utambulisho wa simu laki sita na elfu tatu katika kampeni ya kuondoa simu feki sokoni huku wafanyabiashara wakihangaika kuzihamishia  nchi jirani ambako bado zinatumika ikiwemo Comoro, DRC na Msumbiji.
ITV imetembelea katika maduka mbalimbali yanayouza simu za mkononi na kujionea umati mkubwa wa wananchi wakinunua simu, ambapo akizungumza na ITV mmoja wa wafanyabiashara aliyejitambulisha kwa jina Hamisi Selemani amesema wanunua simu hizo kwa lengo la kuziuza katika nchi hizo ambako zinauwezo wa kufanya kazi.
 
Aidha wamiliki wa maduka ya simu za viganjani wamesema baadhi ya simu hizo ambazo hazina namba tambulishi-imei hazijafungwa na kuitaka mamlaka ya udhibiti wa mawasiliano nchni kufuzifunga ili kuondoa usumbufu kwa wateja na wafanyabiashara.
 
Kwa mujibu wa takwimu za mamlaka ya mawasiliano nchi-TCRA-zaidi ya simu feki za kiganjani laki sita na 30 zimefungiwa mpaka sasa ambapo na inakadiliwa Tanzania asilimia 2.6 ya simu zote zilikuwa feki kati ya watumia simu zaidi ya milioni zaidi ya milioni thelathini na tatu.
 
 
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin