TCRA yawasisitiza wananchi wanaotaka kununua simu mpya wazihakiki kabla ya kununua. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Thursday, June 9, 2016

TCRA yawasisitiza wananchi wanaotaka kununua simu mpya wazihakiki kabla ya kununua.



Siku chache kabla ya zoezi la kuzima simu bandia nchini Juni 16 mwaka huu halijatekelezwa rasmi, mamlaka ya mawasiliano nchini TCRA imewasisitizia wananchi wote nchini wanaotaka kununua simu mpya kwanza wahakiki simu hizo kabla hawajazinunua ili kuwa na uhakika wa kununua simu halisi ama 'feki' kwa vile zoezi hilo liko palepale.
Akizungumza katika mkutano wa kuhitimisha programu ya mwendelezo wa utoaji elimu kwa umma katika suala la uzimwaji wa simu bandia Juni 16 mwaka huu, Mhandisi wa mamlaka ya mawasiliano nchini Mhandisi Imelda Salum licha ya kukiri uwepo wa simu bandia kwenye soko la Mawasiliano lakini amesema suala la kutambua simu bandia ama halisi bado ni changamoto kwa wananchi wengi.
 
Kwa upande wake afisa viwango wa shirika la ubora wa viwango nchini TBS Bw, Safari Fungo amekiri changamoto ya uingizwaji wa simu feki nchini linafanana na la madawa ya kulevya kwavile njia nyingi za panya hutumika lakini amesema kama TBS watahakikisha ukaguzi wa mara kwa mara unafanyika katika soko.
 
Awali akizindua mfumo wa rajisi ya namba za utambulisho wa simu za kiganjani mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikiro pamoja na kuwataka wanaotumia vibaya mitandao ya mawasiliano kuacha kufanya hivyo kwani hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao aliwashauri  wadau wa mawasiliano na viwango kuhakikisha wanadhibiti njia zote zinazotumika kuingiza bidhaa feki nchini.
 
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin