Zaidi ya wanafunzi 3000 wanatumia matundu 2 ya vyoo wilayani Geita. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Thursday, January 28, 2016

Zaidi ya wanafunzi 3000 wanatumia matundu 2 ya vyoo wilayani Geita.


Zaidi ya wanafunzi 3000 wa shule za katoro na uhuru wanatumia matundu mawili ya vyoo kutokana na vyoo vya awali kubomoka hivyo kusababisha usumbufu mkubwa.
Akizungumza na ITV mwalimu mkuu wa shule ya msingi Katoro Paul Enos amesema vyoo hivyo vimebomoka tangu mwaka jana hata hivyo uwingi wa wanafunzi katika shule hizo zilizojirani unatokana na muitikio mkubwa wa wanafunzi kuandikishwa hasa kufuatia ahadi ya rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania kuwa watoto wenye umri wa kwenda shule kuandikishwa.
 
Katika kipindi cha mwaka wa masomo wa mwaka wa 2016,  shule ya msingi Katoro imeandikisha wanafunzi 497 na shule ya Uhuru imeandikisha watoto 590 na bado wanapokea wanafunzi hadi marchi 31,ambapo mwaka jana shule ya msingi Katoro iliandikisha wanafunzi 230 na Uhuru iliandikisha wanafunzi 350 hivyo ongezeko ni kubwa kuliko mwaka jana.
 
Mpaka sasa halmashauri ya wilaya ya Geita imefikia asilimia tisini ya uandikishwaji wanafunzi kwa shule za msingi ambapo, malengo ya uandikishaji kwa mwaka huu ilikuwa ni wanafunzi 26154 lakini mpaka sasa wameandikishwa 23731 na bado wanaendelea kuandikisha.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin