Watu 29 wamelazwa kwa kuugua ugonjwa wa kipindupindu mkoani Manyara. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Friday, January 29, 2016

Watu 29 wamelazwa kwa kuugua ugonjwa wa kipindupindu mkoani Manyara.


Watu 29 wamelazwa katika hospitali ya Mrara ya halmashauri ya mji wa Babati mkoani Manyara baada ya kugundulika kuugua ugonjwa wa kipindupindu, huku wataalam wa afya wakidai kupatwa na hofu ya huenda idadi kubwa ya wagonjwa ikaendelea kuongezeka kutokana baada ya kupokea wagonjwa 18 siku tatu zilizopita na hadi kufikia saa sita mchana ya leo (alhamisi) idadi hiyo imeongezeka toka wagonjwa 28 hadi kufikia 29.
Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Bw Gabriel Sonno Amekiri kupokea idadi hiyo ya wagonjwa na kuthibitisha ukweli kwamba wanasumbuliwa na ugonjwa wa kipindupindu baada ya kufanyika kwa uchunguzi wa kitaalam uliotokana na kupokea wagonjwa wanaohara mfululizo na kutapika, idadi ya wagonjwa 26 wakiwa wanaume na wanawake watatu, huku akisisitiza kwamba hakuna mtu aliyepoteza maisha tangu walipoanza kupokea wagonjwa tangu siku ya jumatatu.
 
ITV imetembelea ndani ya wadi hiyo na kushughudia idadi kubwa ya wagonjwa wengine wakiwa wamelazwa chini na wengine kwenye ukumbi wa ushauri wa akinamama wajawazito na upimaji wa watoto (MCH), huku wagonjwa hao wakieleza chanzo cha ugonjwa wa kipindupindu ni kula kwa mama lishe mmoja kwenye kituo cha mabasi ambaye mpaka sasa wafanyakazi wake watatu wamelazwa huku yeye akisalimika.
 
Nae Bw Faustine Masunga, mkuu wa usafi na mazingira katika halmashauri ya mji wa Babati, amesema licha ya kufunga vibanda vya biashara za vyakula kwa siku 14 na sasa fursa pekee iliyopo ni kusimamia usafi wa mazingira na kusimamia kikamilifu sheria zilizopo ili kudhibiti mlipuko huo ambao haujawahikutokea na kulazwa idadi kubwa ya wagonjwa kama hiyo tangu kuanzishwa kwa mkoa wa Manyara, Julai mosi, 2002.
 
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin