Mgogoro wa ardhi Babati kati ya hifadhi ya jamii na wananchi wapatiwa ufumbuzi. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Friday, January 29, 2016

Mgogoro wa ardhi Babati kati ya hifadhi ya jamii na wananchi wapatiwa ufumbuzi.


Serikali imeanza kuchukua hatua za kumaliza mgogoro wa ardhi uliyo dumu kwa muda mrefu kati ya hifadhi ya jamii ya Burunge na watu wa jamii ya kifugaji wa kabila la Watatoga katika kijiji cha vilima vitatu wilaya ya Babati wanao takiwa kuondoka katika eneo linalodaiwa ni la hifadhi kwa kuwapatia eneo lingine la hekari mia moja arobaini na nne wafugaji hao.
Katika kikao kilicho wakutanisha kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Babati wawakilishi wa wakulima wafugaji na wajumbe wa serikali ya kijiji mkuu wa wilaya ya Babati Crispin Meela amesema baada ya kutafakari kwa muda mrefu athari wanazo zipata wananchi hasa wafugaji serikali imeamua kuwapatia eneo ilo wafugaji ili kumaliza mgogoro uliyo ghalimu muda uhai na uchumi wa binadamu bila sababu ya msingi.
 
Awali kabla ya kauli ya mkuu wa wilaya Mpama ardhi wa wilaya ya Babati Bryceson Shesha alitoa matokea ya kamati iliyoundwa kutazama enelo walilo pewa wafugaji ambalo awali walilikataa kuwa halifai kwa makazi na mifugo na kwamba watalam wamelipitia na kuona kuwa linafaa japo kuna changamoto ndogondogo na wawalishi wa wafugaji nao wakieleza kuridhishwa na hatua hiyo na kutakiwa kupeleka tamko ilo kwa wafugaji waliyo wengi ili nao watambue kinacho endelea.
 
Baada ya makubaliano hayo diwani wa kata ya Nkaiti kutoka Chadema Michael Melau akaitaka serikali kutimiza ahadi hiyo haraka kwani watu wa jamii ya kifugaji katika eneo ilo wameteseka kwa muda mrefu hivyo watendaji wasije wakabadili mpango huo kwa manufaa binafsi.                                                            
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin