Akitoa tathmini ya shughuli za usafi katika mkoa wa Kigoma, mganga
mkuu wa mkoa wa Kigoma Dk Lenard Subi amesema kutokana na kushamiri kwa
kipindupindu mkoani Kigoma kwa miaka mingi, mkoa umeweka mikakati kadhaa
ya kukabiliana na ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa kila
kaya inakuwa na choo na kukitumia baada ya kubainika kaya nyingi hasa za
mwambao wa ziwa Tanganyika hazina vyoo na badala yake watu wanajisaidia
katika ziwa Tanganyika na kwamba kila alhamisi imepangwa kuwa siku ya
usafi katika mkoa wa Kigoma.
Kwa upande wao baadhi ya wananchi wameshauri halmashauri kutunga
sheria ndogo ili kuweka mkazo wa usafi katika kila halmashri na kwamba
jukumu la kupambana na kipindupindu ambacho kimedumu kwa muda mrefu
mkoani Kigoma linapaswa kuishirikisha jamii ili itimize masharti ya
afya.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini