Rais wa Tanzania
John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya
Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Dkt Edward Hoseah, na pia
akawasimamisha kazi maafisa wa nne wa taasisi hiyo.
Rais Magufuli
amesema hajaridhishwa "na namna taasisi hiyo ilivyokua ikitekeleza
wajibu wake katika kukabiliana na rushwa hususani kwenye upotevu wa
mapato ya serikali katika bandari ya Dar es salaam.”
Katibu Mkuu
Kiongozi Balozi Ombeni Sefue amesema Dkt Magufuli amemteua aliyekuwa
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru Bw Valentino Mlowola kuwa Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru.
Kwa mujibu wa Bw Sefue, Dkt Magufuli
amechukua hatua hiyo baada ya kujiridhisha kuwa "utendaji kazi wa
Takururu chini ya Dkt Edward Hoseah hauwezi kuendana na kazi
anayoitaka”.
Rais Magufuli ameagiza kusimamishwa kazi mara moja kwa watumishi
waandamizi wanne wa Takururu ambao walisafiri nje ya nchi licha ya Rais
Magufuli kupiga marufuku safari za nje kwa watumishi wa umma.
Watumishi
hao ni Mary Mosha, Ekwabi Mujungu, Doreen Kapwani na Rukia Nikitas
ambao walisafiri nje ya nchi licha ya kunyimwa kibali cha safari kutoka
kwa Rais ama Katibu Mkuu Kiongozi.
Bw Sefue amesema atakayekiuka agizo la rais "atachukuliwa hatua kali”.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini