Aliyekuwa
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa jimbo la Misungwi, 
Charles Kitwanga (CCM) amezungumzia jinsi alivyopokea kutumbuliwa kwake 
na Rais John Magufuli ambaye anaamika kuwa rafiki yake akisema hawezi 
kuhoji uamuzi huo.
Kitwanga
 aliwaaambia waandishi wa habari nyumbani kwake Misungwi kuwa ingawa 
hawezi kuhoji uamuzi huo, kuna kundi kubwa la wauza madawa ya kulevya 
ndio waliolikuza tukio hilo kwa lengo la kumchongea hadi kuondolewa 
kwenye nafasi hiyo.
“Anayofanya
 Dk. Magufuli nampongeza sana kwani ni mtu ambaye namfahamu. Ni 
mwadilifu, msikivu, namshukuru kwa kuniamini kufanya kazi naye katika 
Serikali yake hivyo siwezi kuhoji alichoamua kwa sababau aliyetoa ndiye 
aliyeondoa,” alisema Kitwanga.
Katika
 hatua nyingine, Mbunge huyo wa Misungwi alikana kuhusika kwa namna 
yoyote katika sakata la kampuni ya Lugumi Enterprises Ltd iliyopewa 
zabuni ya kufunga mashine za kutambua alama za vidole kwenye vituo vya 
polisi nchini, na kudaiwa kulipwa kiasi kikubwa cha fedha wakati kazi 
haikufanyika kama ilivyotarajiwa. Sakata hilo bado lipo katika uchunguzi
 japo dalili za kujadiliwa bungeni zinaonekana kufifia.
“Rais
 wa Kwanza wa Tanzania hayati Mwalimu Julius Nyerere, kuna wakati 
alituhumiwa akidaiwa kuwa na mpango wa kumpindua Rais wa Kenya baada ya 
kuzuru nchini humo. Alipoulizwa na waandishi wa habari alijibu, ‘hivi 
mtu akikwambia mimi ni mume wa mama yako utakubali?’, sasa hilo ndilo 
jibu langu kwa Watanzania ili wasiniulize tena,” alisema Kitwanga.
Akizugumzia
 umiliki wa kampuni ya Infosys, alisema kuwa yeye ni mwanzilishi tu wa 
kampuni hiyo na hivi sasa inamilikiwa na mwanae baada ya kumuuzia 
asilimia 33 ya hisa zake na kwamba taarifa ya mauzo hayo ziko wazi.
 Download Video and Put Comment
 Toa Maoni Hapa Chini
