Zaidi
ya lita 18,000 za pombe haramu ya gongo zimekamatwa wakiwemo watu 30
kwa kujihusisha na upikaji wa pombe hiyo katika wilaya ya Rombo mkoani
Kilimanjaro kati mwezi Aprili na Juni nane mwaka huu na watu hao
watafikishwa mahakamani.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Rombo Bw Evarest Silayo
amesema hayo katika uzinduzi wa albamu ya ngome zimepasuka ya kwaya
nyota ya alfajiri ya kanisa la TAG wilayani humo ambayo pamoja na
kueneza neno la injili lakini pia kwaya hiyo itakuwa inakemea maovu
ndani ya jamii ukiwemo upikaji na unywaji wa pombe hiyo.
Bw Silayo amesema, lita hizo na watu hao wamekamatwa kwa
ushirikiano wa polisi,jeshi la mgambo na raia wema wa wilaya hiyo katika
oparesheni ya kudumu inayofanywa na serikali ili kuhakikisha upikaji na
unywaji wa pombe hiyo unakomeshwa.
Kiongozi wa kanisa hilo Mchungaji Frigili Kimario amesema,kwaya
hiyo pia itajihusisha na kukemea mila potofu katika jamii ukiwemo
ukeketaji kwa wasichana ambao madhara yake ni makubwa na baadhi ya
wanawake wamepoteza maisha katika wilaya hiyo.
Waumini wanawake wa kanisa hilo pamoja na kuipongeza serikali
katika kupambana na pombe hiyo lakini wameiomba iongeze juhudi kwa kuwa
madhara ya pombe haramu ya gongo ni makubwa ikiwemo kupoteza nguvu kazi
ya taifa,ndoa kuvunjika na vijana kukataa kuoa.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini