Vijana mkoani Geita watakiwa kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo yao na taifa. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News

Saturday, June 11, 2016

Vijana mkoani Geita watakiwa kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo yao na taifa.

Vijana wa mkoa wa Geita wametakiwa kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo yao binafsi na taifa kwa ujumla ili kujiondoa katika dimbwi la umasikini ambapo takwimu zinaonyesha kuwa pamoja na mkoa huo kuwa na rasilimali nyingi bado utajiri huo wa madini haujaweza kuwakomboa.
 
Katika kuhakikisha kila mtu anainuka kiuchumi ni lazima umoja na mshikamano wa kazi uwepo kati ya jamii na serikali ambapo wananchi wametakiwa kufanya kazi kwa kufuata sheria na taratibu za nchi huku wananchi wakiiomba serikali kuhakikisha inawaboreshea miundombinu hasa katika sekta ya madini.
 
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Nyakabale kilichopo jirani na mgodi wa dhahabu wa Geita wakiongea mbele ya naibu waziri wa mambo ya ndani wamelilalamikia jeshi la polisi kwa kila wanachokiita uvunjifu wa haki za binadamu pale wanakijiji wanapokuwa katika shughuli zao za kujipatia kipato jirani na mpaka wa mgodi huo.
 
Naye naibu waziri wa mambo ya ndani nchi Ahmad Masauni amesema wizara yake itafuatilia malalamiko yote yaliyotolewa na wananchi pamoja na wabunge wao juu ya ukiukwaji wa haki za binaadamu unaofanywa na askari polisi wakishirikiana na wawekezaji, ili kubaini ukweli na sheria ifuate mkondo.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin