Rais mstaafu wa awamu ya 3 Mh.Mkapa atetea maamuzi yake ya ubinafsishaji. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Tuesday, June 14, 2016

Rais mstaafu wa awamu ya 3 Mh.Mkapa atetea maamuzi yake ya ubinafsishaji.



Rais mstaafu Benjamini Mkapa ametetea uamuzi wake wa kuruhusu ubinafsishwaji wa baadhi ya taasisi za umma, huku pia akikiri baadhi ya kasoro zilizojitokeza wakati wa zoezi hilo ambapo pia ametumia fursa hiyo kuwataka wasomi kuacha kulalamika na badala yake kutumia muda mwingi kufanya tafiti zenye manufaa mapana kwa taifa.
Licha ya kuwataka wasomi kuacha kulalamika, rais mstaafu Benjamini Mkapa pia amewataka wananchi, watendaji pamoja na wabunge kuacha kulalama kwa kutupa kila mzigo kwa serikali na kusema kuwa kila mtu kwa nafasi yake anawajibu wa kuijenga Tanzania.
 
Kuhusu ubinafsishwaji, rais mstaafu Mkapa amesema hapakuwa na tatizo katika zoezi hilo huku akikiri kuwa changamoto kubwa iliyojitokeza ni ukosefu wa chombo cha kusimamia ubinafsishwaji huo, ambapo pia amehoji licha ya serikali kufungua milango ya uwekezaji lakini bado wafanyabiashara wa Tanzania wameshindwa kutumia fursa hiyo na badala yake wameendelea kuwa walalamikaji.
 
Mwenyekiti wa kigoda cha Mwalimu Nyerere Prof Penina Mrama  pamoja na makamo mkuu wa chuo kikuu cha Dar es Salaam Prof Rwekaza Mukandala, wamesema kigoda cha Mwalimu Nyerere kimekuwa kikisaidia kuona namna fikra pevu za mwalimu zinavyopaswa kuenziwa. 
 
Katika siku ya kwanza ya kongamano la 8 la kigoda cha Mwalimu Nyerere chenye kauli mbiu isemayo Mwalimu Nyerere na mtazamo wa kimaendeleo uliojikita katika misingi ya watu, kilihudhuliwa na wasomi, watu mashuhuri na wanadiplomasia, huku viongozi wa nchi za Afrika wakitakiwa kuachana na tawala za kiimla na badala yake  kujenga utaratibu wa kuwasikiliza watawaliwa.
 
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin