TCRA yakutana na wafanyabiashara wa simu na wananchi kutoa elimu juu ya bidhaa feki Lindi. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Tuesday, June 14, 2016

TCRA yakutana na wafanyabiashara wa simu na wananchi kutoa elimu juu ya bidhaa feki Lindi.



Ikiwa zimebaki saa 48 kuzima kwa simu feki hapa nchini, mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA, wamekutana na wafanyabiashara wa simu pamoja na wananchi mkoani Lindi ili kuwapatia elimu juu ya bidhaa hizo feki ambazo zinatarajiwa kusimwa Juni 16 mwaka huu saa sita usiku.
Wakizungumza na ITV baadhi ya wananchi wamesema uzimaji wa simu feki hapa nchini wameupokea kwa mikono miwila ila walio wengi hawajui nini maana ya simu feki huku wakiomba serikali kuwapatiwa elimu juu ya bidhaa hiyo feki ambayo inatarajiwa kuzima siku ya juni 16 mwaka huu.
Kwa upande wao baadhi ya wafanyabiashara wa simu mkoani hapa, wamesema kuzima kwa simu feki ni jambo zuri lakini serikali inatakiwa kudhibiti uingizaji wa bidhaa kwa sasa.
 
Naye mshauri wa masuala ya watumiaji, huduma na bidhaa za mawasiliano kutoka TCRA, Isaac Mruma, amesema baada ya juni 17 mwaka huu tume ya ushindani wa haki na polisi watapita kwenye maduka ya simu kuangalia kama kuna wafanyabiashara ambao bado wanaendelea kuuza simu feki na atakae kutwa sheria kali dhidi yake itachukuliwa.
 
Mamlaka ya mawasiliano nchini TCRA wanatarajia kuzima simu feki ifikapo Juni 16 mwaka huu majira ya saa sita usiku, ambapo wananchi wengi mkoani Lindi hawajui nini maana ya simu feki huku wakiomba serikali kutoa elimu mikoani juu ya vifaa feki ambavyo vimekuwa vikiingizwa nchini na wafanyabiashara mbalimbali.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin