Kiwanda
cha sukari cha TPC kilichopo mkoani Kilimanjaro kimeanza uzalishaji wa
sukari leo ambapo msimu huu wanatarajia kuzalisha tani laki moja na sita
ambazo zitagawanywa kwa wananchi wa mikoa ya kanda ya Kaskazini na
hatimaye kuondoa kabisa tatizo la ukosefu wa sukari sokoni.
Afisa mtendaji mkuu na utawala wa kiwanda cha sukari cha TPC
Bw.Jafary Ally amesema baada ya kumaliza ukarabati na uwekezaji wa
kiwanda hicho ambao uligharimu kiasi cha dola laki tano na nusu,kwa sasa
kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 450 za sukari kila
siku sawa na ongezeko la asilimia 10.
Amesema uzalishaji huo ni mkubwa na kwamba sukari hiyo itaanza
kusambazwa June 18 mwaka huu kwa bei elekezi ambapo mkoa wa Kilimanjaro
utapatiwa tani 100,Arusha tani 100 na Manayara tani 70 na sukari
itakayobaki itasambazwa katika mikoa ya Tanga na Singida.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw.Said Meck Sadick
amesema kwa wasambazaji na wauzaji wa rejereja ambao watakiuka agizo la
kuuza sukari kwa bei elekezi ya serikali watakamatwa na kuchukuliwa
hatua za kisheria.
Baadhi ya wafanyabishara wa sukari mkoani Kilimanjaro wameuomba
uongozi wa kiwanda cha sukari TPC kuangalia uwezekano wa kuruhusu
wafanyabiashara kuchukua sukari kiwandani badala ya mawakala pekee hali
ambayo wanasema itasaidia kuondoa tatizo la sukari kupandishwa bei
hiholela.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini