Siku
mbili baada ya kituo cha ITV kurusha taarifa ya wananchi wa kijiji
cha Likuyumandela kusumbuliwa na Tembo na kusababisha kifo cha
mwananchi mmoja Naibu waziri wa maliasili na utalii amefanya ziara
katika kijiji hicho huku akikiri ziara hiyo imefanyika baada ya kuona
taarifa kwenye kituo cha ITV ambapo ameagiza uchunguzi ufanyike kwa
askari wa wanyamapori aliyesema bora wauawe wananchi mia moja kuliko
Tembo mmoja ili hatua zichukuliwe dhidi yake.
Naibu waziri huyo wa maliasili na utalii Mhandisi Ramo Makani
amefanya ziara ya ghafla akiwasili kwa ndege katika jijiji hicho
baada ya kuona taarifa kwenye kituo cha ITV kuhusiana na wananchi
wanavyosumbuliwa na Tembo ambapo pia ametembelea mashamba ya wananchi
yaliyoharibiwa na Tembo na kwenda kuwapa pole ndugu wa marehemu Yasin
Antonio aliyeuawa kwa kukanyagwa na Tembo huku akilaani kauli ya kwamba
heri wauawe binadamu mia moja kuliko Tembo mmoja.
Mheshimiwa Ramo Makani ameagiza taratibu zifanyike kwa maeneo
mbalimbali nchini kunakotakiwa wananchi kulipwa kifuta jasho na kifuta
machozi taratibu zikamilishwe ili serikali ijue kiasi cha pesa
inachodaiwa huku pia akiagiza taratibu za usajili wa kijiji cha Likuyu
mandela zifanyike na kuagiza kupelekwa kwa askari wanyamapori kwa ajili
ya kufanya doria katika kijiji hicho.
Awali wananchi wa kijiji cha Likuyu mandela chenye wakazi zaidi ya
3500 walieleza malalamiko yao mbele ya naibu waziri huyo wakisema
licha ya wao kuwa mstari wa mbile katika harakati za uhifadhi wa
maliasili lakini viongozi wamekuwa hawachukui hatua wanapopelekewa
malalamiko yao.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini