Chama
cha ACT – Wazalendo kimeelezwa kusikitishwa kwake na kitendo cha jeshi
la polisi cha kuweka ulinzi mkali na kukizuia chama hicho kufanya
kongamano lake katika jengo la Millenium Tower jijini Dar es salaam jana
mchana .
Akiongea na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa ACT – Wazalendo, Mama Anna Mghwira amesema, kitendo hicho ni kuminya demokrasia na kuongeza kwamba, juhudi za kupambana na ufisadi nchini haziwezi kufanikiwa endapo ukandamizaji wa demokrasia utaendelea.
Kadhalika Mama Mghwira anesena, kongamano hilo lililenga kumpa fursa Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia chama hicho, Mh. Zitto Kabwe, kusema yale ambayo angeongea Bungeni hasa baada ya yeye na Wabunge wenzake sita kusimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge la Bajeti.
Akiongea na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa ACT – Wazalendo, Mama Anna Mghwira amesema, kitendo hicho ni kuminya demokrasia na kuongeza kwamba, juhudi za kupambana na ufisadi nchini haziwezi kufanikiwa endapo ukandamizaji wa demokrasia utaendelea.
Kadhalika Mama Mghwira anesena, kongamano hilo lililenga kumpa fursa Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia chama hicho, Mh. Zitto Kabwe, kusema yale ambayo angeongea Bungeni hasa baada ya yeye na Wabunge wenzake sita kusimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge la Bajeti.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini