Serikali yaombwa kutoa elimu kwa wavamizi wa migodi ili wajue madhara yake Geita. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Saturday, April 9, 2016

Serikali yaombwa kutoa elimu kwa wavamizi wa migodi ili wajue madhara yake Geita.

Licha ya wananchi wanaovamia migodi kwa lengo la kuiba madini hapa nchini kuendelea kupoteza maisha bado tatizo hilo limekuwa sugu kwa wananci wanaouzunguka mgodi wa geita huku uongozi wa migodi hiyo ukiendelea kuomba serikali kuongeza jitihada za kusaidia kuwaelimisha wananchi hao ili watambue madhara ya kuvamia migodi.
Akizunguza na ITV Mkurugenzi mtendaji wa mgodi huo amesema tatizo la wavamizi kwenye mashimo ya migodi limekuwa sgu huku wengi wa wananchi wanafanya vitendo hivyo wakiendelea kupoteza maisha ambapo amesema licha ya kufanya vikao na uongozi wa kijiji bado haijasaidia na kuomba serikali kuu kuona nini cha kufanya.
 
Meneja wa uchimbaji wa madini katika migodi ya geita Bwana. Ndibalema Alistides amesema licha ya mgodi huo kutoa ajira kwa vijana wengi wa vijiji vinavyozunguka mgodi huo bado baadhi yao wamekuwa wakiendelea kuvamia licha ya mazingira kutokuwa rafiki na kutoa wito kwa wanachi kuacha mara moja tabia hiyo hatarishi. 
 
Nao baadhi ya wanachi wanaovamia migodi hiyo licha ya kubaini kufahamu madhara ya kuvamia mashimo ya migodi hiyo wamesema wamekuwa wakifanya hivyo kutokana na hali ngumu ya maisha na kutoa wito kwa uongozi wa migodi na serikali.
 
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin