Walimu wakike wanakosa maadili ya mavazi- Msangi | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Tuesday, February 2, 2016

Walimu wakike wanakosa maadili ya mavazi- Msangi


Mkuu wa Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma, Bituni Msangi amesema kuwa baadhi ya walimu wa kike nchini hawavai mavazi yenye maadili ya ualimu hatua ambayo huwasababisha wanafunzi hasa wa kiume kuwataka kimapenzi.
Msangi ambaye pia kitaaluma ni mwalimu ametoa kauli hiyo kwenye hafla iliyoandaliwa na Chama Cha Walimu (CWT) Wilayani Kongwa kwa ajili ya kuwaaga walimu waliostaafu katika Wilaya hiyo.
Amesema kuna baadhi ya walimu wa kike ambao wamekuwa wakikiuka maadili kwa kuvaa mavazi mafupi na ya kubana wawapo kazini hali ambayo huwa inawanyima wanafunzi wa kiume utulivu wa kujifunza ambapo amewaagiza maofisa elimu kuwaeleza walimu wao namna bora ya uvaaji.
Katika hafla hiyo jumla ya walimu 17 waliostaafu walipata zawadi ya mabati 20 kila mmoja waliyopewa na chama cha walimu Wilayani humo.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin