Mkuu wa Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma, Bituni
Msangi amesema kuwa baadhi ya walimu wa kike nchini hawavai mavazi yenye
maadili ya ualimu hatua ambayo huwasababisha wanafunzi hasa wa kiume
kuwataka kimapenzi.
Msangi
ambaye pia kitaaluma ni mwalimu ametoa kauli hiyo kwenye hafla
iliyoandaliwa na Chama Cha Walimu (CWT) Wilayani Kongwa kwa ajili ya
kuwaaga walimu waliostaafu katika Wilaya hiyo.
Amesema kuna baadhi ya walimu wa kike ambao wamekuwa wakikiuka maadili kwa kuvaa mavazi mafupi na ya kubana wawapo kazini hali ambayo huwa inawanyima wanafunzi wa kiume utulivu wa kujifunza ambapo amewaagiza maofisa elimu kuwaeleza walimu wao namna bora ya uvaaji.
Katika hafla hiyo jumla ya walimu 17 waliostaafu walipata zawadi ya mabati 20 kila mmoja waliyopewa na chama cha walimu Wilayani humo.
Amesema kuna baadhi ya walimu wa kike ambao wamekuwa wakikiuka maadili kwa kuvaa mavazi mafupi na ya kubana wawapo kazini hali ambayo huwa inawanyima wanafunzi wa kiume utulivu wa kujifunza ambapo amewaagiza maofisa elimu kuwaeleza walimu wao namna bora ya uvaaji.
Katika hafla hiyo jumla ya walimu 17 waliostaafu walipata zawadi ya mabati 20 kila mmoja waliyopewa na chama cha walimu Wilayani humo.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini