Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Saidi Mecky Sadiki ametoa agizo hilo
mara baada ya kutembelea eneo hilo ambapo amesema lengo la wao kutakiwa
kuondoka ni kunusuru maisha yao na kwamba baadhi ya barabara nazo
zitafungwa huku akielezea sababu zilizochelewesha zoezi hilo la ubomoaji
kuanza.
Baadhi ya wananchi wanaotakiwa kupisha zoezi hilo wamepongeza hatua
hiyo na kudai kuwa walikuwa wanaishi kwa mashaka kwa kipindi chote
hicho na wengine wakihoji utaratibu wa gharama za kuhama kwa madai kuwa
hawana uwezo wa kwenda kupangisha hoteli miezi yote hiyo.
Akizungumzia zoezi hilo mkurugenzi wa manispaa ya Ilala Bw Isaya
Mngulumi amesema baada ya kikao cha ulinzi na usalama cha mkoa
kumalizika wanatoa taarifa ya maandishi kwa wakazi hao ya kuhama huku
mhandisi mshauri wa kampuni iliyopewa tenda ya kulibomoa akielezea namna
watakavyolibomoa bila ya kutumia mashine au baruti.
Uamuzi wa kubomoa jengo hilo umechukuwa zaidi ya miaka mitatu tangu
lilipobainika kuwa limejengwa chini ya kiwango na halikuzingatia vibali
vya ujenzi kwani lilipewa kibali cha kujenga ghorofa 10 badala yake
wakajenga ghorofa 16.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini