Zaidi ya mbao 250 zakamatwa zikisafirisha kwa Jahazi kutoka Rufiji kwenda Zanzibar. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Tuesday, January 26, 2016

Zaidi ya mbao 250 zakamatwa zikisafirisha kwa Jahazi kutoka Rufiji kwenda Zanzibar.

Zaidi ya mbao 250 zilizokuwa zikisafirishwa kutokea Rufiji kwenda visiwani Zanzibar kinyemela kwa kutumia usafiri wa Jahazi kupitia baharini, zimekamatwa na jeshi la polisi kikosi cha wana maji katika eneo la Buyuni umbali wa kilometa mia moja kutokea jijini Dar es Salaam na kuzirejesha.
ITV imeshuhudia mbao hizo zikiwa tayari zimefikishwa katika makao makuu ya polisi kikosi cha wana maji huku vijana waliokuwa wakisafirisha mbao hizo kutokea Rufiji kuelekea visiwani Zanzibar nao wakiwa wameshikiliwa na jeshi hilo ambapo kamanda wa kikosi cha wana maji nchini kamishna msaidizi mwandamizi wa jeshi la polisi Mboje John Kanga ameeleza walivyofanikiwa kukamata mbao hizo.
 
Aidha kamanda kanga, amewataka wenye tabia ya kusafirisha mizigo ya aina yeyote kwa kutumia njia ya bahari au ziwa kinyemela ili kukwepa kodi kuacha mara moja kwani hata majira ya usiku jeshi hilo ufanya kazi zake baharini na kwenye ziwa.
 
Meneja misitu kutoka wakala wa misitu wilaya ya Ilala Bwana Doto Ndubikwa amesema iwapo mwenye mali hiyo hatajitokeza kwa kipindi kilichowekwa basi mali hiyo itataifishwa kwa maslahi ya umma huku vijana hao walioshikiliwa wakieleza walivyokuwa wakisafirisha mbao hizo na kwamba mwenye mali anaitwa Temri huku wakieleza malipo waliyoahidiwa.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin