Wafanyabiashara 28 wa gongo mkoani Manyara wanusurika kushambuliwa na wananchi wenye hasira | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Friday, June 10, 2016

Wafanyabiashara 28 wa gongo mkoani Manyara wanusurika kushambuliwa na wananchi wenye hasira


.
Takribani wafanyabiashara 28 wanaodaiwa kujihusisha na biashara ya pombe haramu ya Moshi maarufu kama Gongo katika kijiji cha Barjomod wilayani Hanang mkoani Manyara wamenusurika kushambuliwa na kubomolewa makazi yao sambamba na kufukuzwa kijijini hapo na wananchi zaidi ya 500 wenye hasira baada ya kugundulika kukiuka sheria ndogo ya kijiji na kuendelea kuuza pombe hiyo iliyosababisha vifo vya watu watano.
ITV ilishuhudia msako huo wa nyumba kwa nyumba, shamba kwa shamba maeneo yanayoaminika kufanyika na kufichwa kwa pombe hiyo ambayo baadhi ya wazee wa mila na desturi wamesema imechangia kudhoofisha nguvu kazi kwa vijana na kushindwa kuoa, familia kutelekezwa, vipigo kwa wanawake, vifo na kushuka kwa maadili.
 
Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho cha Barjomod kilichopo kata ya Gitting Bw William Basso mbele ya mkutano ulioitishwa na wazee wa mila anasema msako huo umedumu kwa siku saba usiku na mchana na wamelazimika kuwatoza wafanyabiashara tozo la Ng’ombe 30 wakiwemo wenyeviti wa vitongoji walioshindwa kudhibiti biashara hiyo na mifugo hiyo wamekuwa wakifanya karamu badala ya kuuza.
 
Hata hivyo mkuu wa wilaya ya Hanang Bw Thobias Mwilapwa alipoulizwa juu ya uhalali wa tozo hilo amesema kulingana na wazee hao wa mila na desturi wanalenga kukomesha uhalifu kupitia biashara hiyo inayosababisha vifo amesema lazima wazingatie sheria za nchi.
 
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin