Inahitajika nidhamu ya hali ya juu sana kifikra na kimaamuzi, 
kutoyumbishwa na habari zinazovuma kila kukicha katika taifa letu kwa 
sasa. Juzi UKUTA, jana kupatwa kwa jua, leo noti mpya kuchapishwa, kesho
 mtu kakamatwa kwa kumtukana Rais, hujakaa sawa mara wanafunzi hewa!
 Ukiamua kukisemea kila kinachosikika utajitia "stress" zisizo na sababu
 na utapoteza uelekeo. Huu ndio wakati unaohitaji kujipambanua na 
kujidhibiti, kwa sababu kinyume na hapo unaweza kugeuka mbwa 
unaehangaishwa na mifupa inayorushwa kila siku.(tena mingine kwa 
makusudi kukupoteza na kutafuta huruma zako). Ndio maana kwa sasa 
nimeamua kutohangaika kabisa na taarifa za habari hasa za kwenye TV!
 Kila siku ninashangilia maisha (huwezi kunikuta nikilalamika hata kwa 
bahati mbaya), kwa sababu ninajua(kwa uhakika kabisa) kwamba mabadiliko 
yamelifikia taifa kwa ajili ya manufaa yangu! Full stop! Mengine wanajua
 wenyewe wanaohusika nayo, hayanihusu!
 Download Video and Put Comment
 Toa Maoni Hapa Chini
 

 
 
 
