Mgeni
 Rasmi Tamasha la Ajira na Ujasiriamali Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya 
Makamu wa Rais Mazingira na Muungano Mh Luhanga Mpina Akikagua Maonyesho
 ya Kazi Mbalimbali Kwenye Tamasha la Ajira na Ujasiriamali 
Lililofanyika Chuo Kikuu Mzumbe Mkoani Mbeya.
Katika
 kutengeneza Msingi Mzuri kwa Wanafunzi wake na kuwajengea uwezo Chuo 
Kikuu cha Mzumbe kampasi ya Mbeya kilifanya maonyesho makubwa ya Ajira 
na Ujasiriamali siku yatarehe 11 June 2015 mjini Mbeya. Tukio hilo la 
aina yake, pia lilishirikisha wanafunzi wa vyuo wingine vya nyanda za 
juu kusini.
Afisa Mtendaji Mkuu waEAG group Imani Kajula Akitoa Mada kwenye Tamasha La Ajira na Ujasiriamali Lililofanyika Mkoani Mbeya
Upatikanaji
 wa ajira za uhakika imekuwa changamoto kubwa sana kwa vijana wengi 
wanaomaliza vyuo Nchini Tanzania hivyo ujasiriamali ni njia moja muhimu 
ya kutatua changamoto hiyo.Wanafunzi wengi walioshiriki walieleza Furaha
 yao kwa Maonyesho hayo. Mgeni rasmi Mh.Mpina aliwataka Wanafunzi 
kutumia fursa zilizopo kujiletea Maendeleo na kujiajiri.
Mkurugenzi
 wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media Group Ruge Mutahaba  Ambaye naye 
alitoa Mada Mbalimbali Namna ya Kukabiliana na Changamoto ya Ajira Hapa 
Nchini
Katika
 kufanikisha siku hiyo wataalam na wabobeaji wa biashara na fursa za 
ajira walialikwa kutoa mada na kushare uzoefu wao kwenye ujasiriamali na
 utendaji kazini. Watoa
 mada walio alikwa kwenye kongamano hili kubwani; Imani Kajula ambaye ni
 Mkurugenzi Mtendaji wa EAG Group, Ruge Mutahaba ambaye ni Mkurugenzi wa
 Vipindi na Uzalishaji Clouds Media Group. Wakili Alberto Msando 
– Wakili maarufu wa kujitegemea na Mjasiriamali, Victor Kikoti 
Compliance Manager – LAPF na Ephraim Lwila – Meneja wa Tawi la CRDB 
Mbeya. Mgeni Rasmi wa Kongamano hilo alikuwa Naibu Waziri wa Mazingira 
na Muungano Mh.Luhaga Mpina.
Washiriki
 wa Tamasha Hilo wakisikiliza Kwa Makini Mda Mbalimbali Zilizowasilishwa
  Kwenye Tamasha la Ajira na Ujasiriamali Lililofanyika Chuo Kikuu 
Mzumbe Kampasi ya Mbeya
Pia
 katika kuhitimisha siku hiyo, Timu za wanafunzi wa Mzumbe Mbeya na TIA 
Mbeya walicheza Mechi ya mpira wa miguu, ambapo chuo cha Mzumbe 
kiliifunga TIA kwanjia ya penati. Mkurugenzi wa EAG Group Imani Kajula 
alikabidhi zawadi kwa timu zote mbili.
 Download Video and Put Comment
 Toa Maoni Hapa Chini
 
 
 
 
