Tangu
wabunge wa upinzani waanze kususa vikao vinavyoongozwa na Naibu Spika,
Dk Tulia Ackson, kiongozi huyo wa Bunge ameamua ‘kukomaa’ na kiti hicho,
hatua inayosababisha wapinzani wasipate fursa ya kutia mguu bungeni.
Kwa
kawaida, Spika wa Bunge, Job Ndugai au naibu wake wanapokuwa na
shughuli nyingine, huachia kiti hicho kwa wenyeviti watatu wa Bunge
kuendesha vikao, lakini safari hii Dk Tulia amekuwa akiingia kila siku
asubuhi na jioni.
Mei
31, mwaka huu wabunge wote wa upinzani walianza kususa vikao
vinavyoendeshwa na kiongozi huyo kwa madai ya kutokuwa na imani naye,
hasa baada ya kuzuia hoja ya kufukuzwa kwa wanafunzi 7,802 katika chuo
cha Udom.
Hoja
hiyo iliwasilishwa na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari
lakini Dk Tulia alisema haikuwa na umuhimu kwa wakati huo, jambo
lililozua tafrani baina ya kiongozi huyo na wabunge wote wa upinzani.
Kutokana
na hali hiyo, wabunge hao walipitisha azimio la kususa vikao
vinavyoendeshwa na kiongozi huyo na tangu siku hiyo, kila anapoingia
bungeni kuongoza kikao wamekuwa wakitoka ukumbini.
Spika
wa Bunge, Job Ndugai ambaye kwa sasa yuko nchini India kwa matibabu,
amekuwa akisaidiwa na Dk Tulia pamoja na wenyeviti watatu wa Bunge ambao
ni Mbunge wa Ilala (CCM), Mussa Azzan Zungu, Mbunge wa Bariadi Andrew
Chenge
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini