Kamati ya bunge ya bajeti imeishutumu serikali kwa kupuuza ushauri wake katika kuboresha bajeti 2016/17. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Friday, June 10, 2016

Kamati ya bunge ya bajeti imeishutumu serikali kwa kupuuza ushauri wake katika kuboresha bajeti 2016/17.



Kamati ya bunge ya bajeti  imeishutumu serikali kuwa  imekuwa haiiamini  na kwa kiasi kikubwa katika bajeti ya mwaka huu  ushauri  ambao imekuwa  ikitoa umekuwa ukipuuuzwa   hatua ambayo  imesema  ni  ishara ya  kutaka  kulirudisha bunge   kuwa muhuri katika kuidhinisha  bajeti  ya  mwaka huu.
Akisoma hotuba   ya  kamati hiyo bungeni  mwenyekiti wake mh hawa ghasia  amesema serikali imekuwa  haipokei  ushauri wa vyanzo vipya  vya  mapato  ambavyo wamekuwa wakishauri.
 
Kwa upande wake  naibu waziri  kivuli  na msemaji mkuu wa kambi ya upinzani bungeni  katika wizara ya fedha  na mipango mh.david silinde  amesema  hawana  tatizo   na mpango  wa serikali wa kutaka  kukata kodi  asilimia  tano  kwenye kiinua mgongo  cha wabunge  ambapo kambi hiyo ya uapinzani baada ya kuwasiliasha hotuba yao  pia walifanya mkutano na waandishi habari  na kufafanua kuhusu bajeti hiyo , mh james mbatia  anasema.
 
Baadhi   ya   wabunge wakichangia  bajeti  hiyo  wamesema  bajeti  iliyowasilishwa  imegusa sehemu nyingi  na  itaweza  kuwafikisha  wananchi  jambo  la  muhimu ni kila mtu kuhakisha anajitahidi  kulipa kodi ili bajeti iweze  kutekelezeka.
 
Katika hatua  nyingine naibu spika dk tulia ackson  ameielekeza  kamati  ya  haki maadili na madaraka ya bunge kinga na maadili ya  bunge  kuchunguza na kutolea  uamuzi kitendo kinachodaiwa  kufanywa na mh joseph  mbilinyi mbunge wa mbeya  mjini cha  kuonyesha kidole la kati  hatua  ambayo imetafisiriwa kama ni  kulidhihaki  bunge.
 
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin