Jukwaa la katiba lamuomba Rais Magufuli kutaja tarehe rasmi ya kuanza mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Thursday, June 16, 2016

Jukwaa la katiba lamuomba Rais Magufuli kutaja tarehe rasmi ya kuanza mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya.



Jukwaa la katiba Tanzania limemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli kutaja tarehe rasmi ya kuanza mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya katika serikali ya awamu ya tano ili kuanza mapema katika mwaka wa fedha unaoanza julai mosi mwaka huu.
Akiongea na waandishi wa habari mwenyekiti wa bodi ya  jukwaa la katiba Bw.Deusi Kibamba amepongeza jitihada za Rais Magufuli za kubana matumizi serikalini hivyo basi ametumia fursa hiyo kuomba  mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya kuanza  kutokana na kugharimu fedha kiasi cha zaidi ya bilioni 100 bila kufikia malengo.
 
Katika hatua nyingine Ebron Mwakagenda amesema wananchi wako na uhitaji wa katiba mpya iliyoainisha mambo muhimu yanayowagusa na kutatua changamoto walizo nazo.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin