RAIS MAGUFULI AMEMTEUA BW. GELASIUS GASPAR BYAKANWA KUWA MKUU WA WILAYA YA HAI. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Friday, April 8, 2016

RAIS MAGUFULI AMEMTEUA BW. GELASIUS GASPAR BYAKANWA KUWA MKUU WA WILAYA YA HAI.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bw. Gelasius Gaspar Byakanwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Mkoani Kilimanjaro.

Taarifa iliyotolewa leo Ikulu Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, imeeleza kuwa uteuzi huo umeanzia tarehe 08 April, 2016. Bw. Byakanwa anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Antony Mtaka aliyeteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.

Kabla ya Uteuzi huo, Bw. Byakanwa alikuwa Katibu wa Rais Msaidizi Mwandamizi.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es Salaam
08 Aprili, 2016
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin