Wilaya
ya Same mkoani kirimanjaro inakabiliwa na upungufu wa walimu 200 wa
masomo ya sayansi katika shule za sekondari hali ambayo imesababisha
wanafunzi kushindwa kufanya vizuri kitaaluma na hivyo kuisababisha
wilaya hiyo kushika nafasi ya mwisho kimkoa.
Afisa elimu sekondari wilaya ya Same Bi Happynes Laizer amesema
walimu wengi wanaopangiwa kufanya kazi katika wilaya hiyo wamekuwa
hawaripoti kutokana na jiografia ya wilaya hiyo kuwa na milima.
Amesema wanafunzi wengi wanakata tamaa kutokana na ukosefu wa
walimu, wanafunzi kutembea umbali mrefu na ukosefu wa vifaa vya
kufundishia hali ambayo inasababisha kiwango cha taaluma katika wilaya
hiyo kuzidi kushuka kila mwaka.
Walimu wanasema wanafunzi walio wengi hawana utamaduni wa kujisomea
kutokana na wilaya hiyo kutokuwa na maktaba, pamoja na ukosefu wa
vitabu vya kutosha mashuleni hali inayochangia wanafunzi wengi kushindwa
kufanya vizuri kitaaluma.
Nao baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kwakoko wilayani
Same ambao wamepatiwa kompyuta ndogo za mkononi zenye vitabu vya
kujifunzia wanasema kwa sasa wana uhakika wa kufanya vizuri kitaaluma.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini