MaliI
 zenye thamani ya Sh bilioni sita za baadhi ya wadaiwa 16, waliokwepa 
kulipa kodi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), baada ya kutorosha 
kontena za mizigo yao kwenye Bandari Kavu (ICD) ya Azam mwishoni mwa 
mwaka jana, zimekamatwa jana na zinafilisiwa.
Aidha,
 mali nyingine za thamani ya Sh bilioni 7.4 zimebainishwa na muda wowote
 kuanzia leo zitakamatwa ili kufilisiwa kwa lengo la kulipa kodi 
inayodaiwa na TRA.
Hayo
 yalibainishwa Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya 
Udalali ya Yono, iliyopewa kazi ya kufuatilia wadaiwa hao, Yono Kevella 
alipokuwa akizungumzia kuanza kwa kazi ya kukamata mali za wadaiwa hao 
na kufilisiwa.
Kevela
 alisema baada ya kuisha muda wa siku 14, walioutoa kwa wadaiwa 24 
kulipa madeni yao ya Sh bilioni 18.95, hadi juzi ni wadaiwa nane tu 
waliweza kulipa, hivyo hao 16 hawakulipa na mali zao ndio zimeanza 
kukamatwa na kufilisiwa.
Aliwataja
 wadaiwa ambao mali zao zimekamatwa na wamekubali wenyewe zifilisiwe 
kulipa deni hilo kuwa ni Tifo Global Trading Co Ltd wanaodaiwa Sh 
bilioni 1.57 na Lotai Steel Tanzania Ltd wanaodaiwa Sh bilioni 5.47.
Alisema wadaiwa hao ni wawekezaji kutoka China na wamekubali kwa hiari yao mali zao zifilisiwe kulipa deni wanalodaiwa. 
Mali zilizokamatwa na ziko tayari chini ya kampuni hiyo ya Yono ni kontena tisa za mabati, zenye thamani ya Sh bilioni sita.
"Nitumie
 fursa hii kuwaalika wananchi wote wanaohitaji mabati waje ofisi za 
kampuni yetu kununua mabati hayo, yako mengi ni kontena tisa, 
tunachofanya si kumuonea mtu, bali tunatekeleza wajibu wetu tuliopewa wa
 kuhakikisha kodi ya serikali inalipwa”, alisema Kevella.
Alisema
 kazi ya kukamata mali za wadaiwa wengine 14, zinaendelea na ndani ya 
wiki moja kazi hiyo itakuwa imekamilika na iwapo wahusika wote 
hawatapatikana, Kampuni ya SSB ambayo ndiyo mmiliki wa bandari kavu ya 
(Azam ICD) na kampuni ya wakala wa forodha ya Regional Cargo Services, 
watahusika kulipa deni linalobaki.
"Kwa
 wale tutakaoshindwa kuwapata au kukamata mali za kutosha kulipa deni 
wanalodaiwa, mmiliki wa bandari kavu ya Azam ICD, na kampuni ya wakala 
wa forodha ya Regional Cargo Services, watapaswa kulipa”, alisisitiza Kevella.
Kevella
 alisema jana jioni walitarajia kukamata mali nyingine za Sh bilioni 7.4
 za mdaiwa Tuff Tyres General Co Ltd, ambaye amekimbilia kufungua ombi 
mahakamani lakini Mahakama haijatoa uamuzi.
Alisema
 wameshazibainisha mali za mdaiwa huyo, ikiwa ni pamoja na jengo la 
ghorofa, matairi na nyumba iliyopo Msasani, ambazo zote kwa pamoja 
zikifilisiwa zitalipa deni la Sh bilioni 7.4 anazodaiwa.
 Download Video and Put Comment
 Toa Maoni Hapa Chini
