Akizungumza na ITV meneja wa shamba hilo Bwana Patric Anthoni
amessema anashangazwa na hatua ya mkuu wa wilaya ya Kilosa kushindwa
kuheshimu maamuzi ya mahaka kwa kuwaruhusu wananchi kuendelea na
shughuli za kilimo katika shamba la kampuni jambo ambalo linaweza
kusababisha uvunjifu wa amani.
Nao wasimamizi wa shamba wamesema walivamiwa na kundi la wananchi
wakidai kuagizwa na mkuu wa wilaya ya Kilosa kuhakikisha wanalinda
shamba hilo ambapo kufuatia uvamizi huo jeshi la polisi kikosi cha
kutuliza ghasia kimefika katika shamba la mwekezaji huyo na kukuta
wananchi wamekwisha tawanyika na hivyo kuimarisha ulinzi katika shamba
hilo.
Akizungumza kwa njia ya simu mkuu wa wilaya ya Kilosa Bwana John
Henjewele amesema muwekezaji huyo kama ana malalamiko ya msingi afuate
ngazi za kisheria ili malalamiko yake yaweze kufanyiwa kazi na sio
kulalamika kwenye vyombo vya habari.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini