Mvua kubwa yaharibu miundombinu na baadhi ya nyumba wilayani Meatu. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Wednesday, February 3, 2016

Mvua kubwa yaharibu miundombinu na baadhi ya nyumba wilayani Meatu.


Mvua kubwa iliyonyesha jana mjini Mwanhuzi wilayani Meatu takribani masaa mawili imesababisha kuharibu miundo mbinu ya barabara na daraja kumeguka na kuleta adha kubwa kwa abiria waliokuwa wakisafiri kutoka Mwanhuzi kuelekea Mwanza, Shinyanga, Maswa na Bariadi na baadhi ya kulala katika eneo hilo, huku wengine wakiwa ni wagonjwa wakiwahi hospitali na kuiomba serikali kupitia wakala wa barabara mkoa wa Simiyu kuirejesha huduma hiyo mapema.
ITV imeshuhudia msururu wa magari ya abiria na malori zaidi ya kumi yaliyolala jana kutokana na kuharibika kwa barabara hiyo huku basi la kampuni ya Hokas lililonusurika  kutumbukia mtoni na kuweza kuziba barabara  hivyo kulingana na ufinyu wa barabara na kumeguka kwa kuta ambapo kilio chao kikubwa wasafiri hao ni kuiomba serikali kuifanyia marekebisho ya dharura barabara hiyo mapema diwani wa kata ya Mwanahuzi, Elias Shukia amesema wananchi waliokolewa nyumba zao wanahitaji msaada wa haraka kwani wengine kwa sasa hivi.
 
Aidha wananchi hao wameishauri serikali kulipanua daraja la mto huo kwani mkubwa ambapo daraja lililowekwa ni finyu na kulingana na maji kujaa mara kwa yamekuwa yajichimba kila kukicha.
 
Akiongea na ITV kwa njia ya simu meneja wa wakala wa barabara, Tanroad mkoa wa Simiyu Albert Kenti amesema tayari ameshaandaa mitambo na vifaa kwa ajili ya kupeleka eneo la tukio ili kuanza kazi ya matengenezo ya barabara hiyo ili kuweza kuruhusu magari yaweze kupita.
 
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin