Jaji
Mkuu wa Tanzania, Othuman Chande (katikati), akizungumza katika mkutano
na waandishi wa habari (hawapo pichani), Dar es Salaam leo mchana ,
kuhusu utendaji wa mahakimu wa mahakama za hakimu mkazi, mahakama za
wilaya na mahakama za mwanzo ambapo alitoa siku saba kwa mahakimu 508
watoe maelezo kwani ni wasifunguliwe mashitaka ya nidhamu na
kuwajibishwa kwa kufanya kazi chini ya kiwango.
Kushoto
ni Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omari Mallungu na kulia ni Jaji Kiongozi wa
Tanzania, Shaban Omari Lila. Jaji Chande alitoa kauli hiyo kwenye
maonyesho ya wiki ya Sheria yanayoendelea viwanja vya Mnazi Mmoja.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Othuman Chande, akikaribishwa kutembea mabanda mbalimbali kwenye maonesho hayo.
Mkurugenzi
Msaidizi Ukaguzi na Maadili Mahakama ya Tanzania, Warsha Ng'humbu
(kushoto), akimuelekeza jambo Balbina Mrosso (kulia), kutoka Babati
mkoani Manyara aliyetembelea banda la Idara ya Malalamiko kuomba msaada
wa kisheria katika maonyesho hayo
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini