Wakazi wa kilombero waiomba serikali kutatua mgogoro kati yao na poli Tengefu. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Tuesday, January 26, 2016

Wakazi wa kilombero waiomba serikali kutatua mgogoro kati yao na poli Tengefu.


Wakulima na wafugaji wa wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro wameiomba serikali iwasaidie kuainisha na kuweka mipaka ya kudumu kati ya wananchi na pori Tengefu la bonde la mto Kilombero ili kuondoa migogoro iliyopo ya wananchi kuvamia na kufanya shughuli za kilimo na ufugaji katika pori hilo.
Wakizungumza katika kijiji cha Msolwa na kijiji cha Namwawala wananchi hao wametupia lawama uongozi wa wilaya ya Kilombero kwa kuwapiga wananchi na kuwatoza faini ya shilingi elfu 50 kila mfugo ingawa pamoja na hayo halmashauri hiyo haitaki kumaliza mgogoro huo wa mipaka uliopo baina ya wananchi na pori Tengefu la bonde la mto Kilombero.
 
Naye mwenyekiti wa kijiji cha Msolwa Bwana Salum Malila amesema makubaliano ya wanakijiji na mradi wa ramsa walikubaliana kuacha mita 60 kutoka mipaka ya pori badala yake waliamua kuacha mita 100 ili kuepusha migogoro lakini bado uongozi wa wilaya unaendelea kuwanyanyasa na kwamba hawapo tayari kuona ardhi yao inamilikiwa na viongozi wachache bila sababu.
 
Akijibu malalamiko ya wananchi hao mkuu wa wilaya ya Kilombero Bwana Lefy Gembe amesema pori hilo lipo kwa mujibu wa sheria na hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kufanya shughuli za kibinadamu katika eneo hilo ingawa kuna makundi makubwa ya mifugo na mashamba mengi yawakulima na kwamba atafanya operesheni maalumu kuhakikisha hakuna mtu yeyote anayebaki ndani ya pori hilo.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin