Mfalme wa muziki wa taarab, Mzee Yusuph
amefunguka na kusema hataki kusikia siasa wala hataki kugombea nafasi
yoyote ile ya uongozi, Mzee Yusuph aliyasema haya jana kupitia kipindi
cha Tam tam za Mwambao cha East Africa Radio.
Mzee
Yusuph mwaka jana alikuwa na nia ya kugombea ubunge kupitia tiketi ya
Chama cha Mapinduzi katika jimbo la Fuweni Zanzibar lakini baadaye
alipigwa chini kwenye kura za maoni na badala yake alikuwa akionekana
kwenye kampeni za chama hicho akitoa burudani kama ambavyo wasanii
wengine walikuwa wakifanya.
"Sahizi nasema ukweli kabisa sitaki kusikia kitu kinaitwa siasa, na wala mwaka 2020 siwezi kugombea nafasi yoyote ile ya uongozi labda itoke nichaguliwe tu ila mimi na siasa hapana, kwa sasa mimi nataka kuangalia masuala ya biashara niwe mfanyabiashara mkubwa kama wakina Dr Reginald Mengi, Azam, Mo Dewji yaani nataka kushindana na watu hawa kibiashara ila sio siasa sitaki kusikia kabisa". Alisema Mzee Yusuph.
"Sahizi nasema ukweli kabisa sitaki kusikia kitu kinaitwa siasa, na wala mwaka 2020 siwezi kugombea nafasi yoyote ile ya uongozi labda itoke nichaguliwe tu ila mimi na siasa hapana, kwa sasa mimi nataka kuangalia masuala ya biashara niwe mfanyabiashara mkubwa kama wakina Dr Reginald Mengi, Azam, Mo Dewji yaani nataka kushindana na watu hawa kibiashara ila sio siasa sitaki kusikia kabisa". Alisema Mzee Yusuph.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini